Saturday, January 3, 2015

SEKESEKE LA PANYA ROAD: JIONEE VITUKO VYA MZEE MAJUTO NA NISHA

Kama mnavyojua, siku ya jana hapa jijini Dar es salaam kulikuwa na taharuki kubwa  ikiwahusisha baadhi ya vijana wanaojikusanya kwenye vikundi na kujiita Panya road  ambao huzunguka mitaani kufaya vurugu na kupora watu na hivyo kusababisha hofu kubwa kwa wakazi wa jijini hapa.
Hivi ni vituko vya waigizaji Mzee Majuto na  Nisha kwa nyakati tofauti, Mzee Majuto akiwa nje ya jiji la Dar, akionekana  “anagonga”  mchemsho wa samaki huku anaongea na simu, JB alimuwekea maneno haya kwenye picha hiyo;
 Hallow poleni sana Dar na panya road.Huku ni raha tu.poleni sanaaa.hahaha
Hii iliwavunja mbavu watu kibao huko mtandaoni nakupokea 'Likes' za kutosha.
Wakati  wigizaji Nisha akiwa amebebelea  silaha  mbalimbali, kama panga, shoka  na kuzitupia video na picha mabilmbali mtandaoni na kuandika kuwa yupo kwenye msako kuwatafuta hao panya road.
Mwishoni akatupia picha hiyo na kuandika “Wakijitokeza tena mnibeep 000000
Ila wengi walisema kama Nisha anaogopa , na kama wangetokea hapo angetoka nduki....wewe umemuonaje hapo, angewaweza kweli?.