Monday, May 4, 2015

POMBE SIO SUPU...Sharabaro anusurika Kubonyezwa kizenji ......Picha za tukio

Sharobaro huyo akiwa amelala chini hajielewi.

Noma sana! Kijana mmoja ‘sharobaro’ ambaye jina halikufahamika amenusurika kufanyiwa kitu mbaya ‘kubonyezwa kizenji’ na wahuni baada ya kupiga mitungi na kuwa chakari.
Sharobaro huyo akiwa kajitapikia chini na akiwa amelala huku akiwa hata hajitambui.
Tukio hilo la kusikitisha lilijiri juzikati ambapo jamaa huyo alikutwa kwenye kichaka maeneo ya Holowela, Mji Mpya mkoani hapa huku suruali ikiwa magotini.
Sharobaro huyo akiwa amelala hajitambui.
Wakizungumza na Ijumaa wikienda, mashuhuda wa tukio hilo walieleza kwamba, kijana huyo mtanashati alionekana kuzidiwa na kilevi kisha kuangusha gari’ mahali hapo.
“Tulikuwa tunatoka kwenye kigodoro mishale ya saa 7:00 usiku.
“Tulipofika hapa tumemkuta huyu jamaa akiwa kwenye hiki kichaka akionekana kulewa.
“Baada ya kumchunguza tumeshindwa kumtambua kwani siyo mkazi wa mtaa huu hivyo wahuni wanaweza kumfanyia chochote,” alisema mmoja wa mashuhuda hao aliyejitambulisha kwa jina la Shaban Madodo.