Tuesday, June 23, 2015

Video: Zitto Kabwe azomewa Tunduma, aitwa Yuda na Msaliti, akiri kuonja supu ya jiwe Tunduma

Ule usemi wa Mla kuku wa mwenziwe miguu humuelekea, imetokea leo Tunduma wakati kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo alipoenda kueneza chama kwa kuikashifu CHADEMA. Hapo ndo nikaamini ule usemi kwamba, Mkataa pema pabaya pamuita. Akakumbuka usemi alokua akiusema alipokua CHADEMA wa CHADEMA ilipo ilifanya kazi ndo akakumbuka Ukimwona nyani mzee, amekwepa mishale mingi

Zitto akakumbuka jinsi alivokua anafunga barabara kwa kujaza watu aingiapo Tunduma kipindi akiwa CHADEMA na Sasa anapotafuta watu kwa tochi, ikambidi ajiinamie huku kashikilia mlingoti wa bendera ya ACT na kujisemea kimoyomoyo, "Ningejua nisingekuja Tunduma bila kujali ningejua ni kiapo cha mjinga na huja baada ya tendo.

Mimi sitaki kuwawekea picha za photoshop wala za kuchakachua ya Kigoma niilete Tunduma, hapana. Nimeamua kuwawekea video ili Wabishi na wagumu wa kuelewa wakose la kusema na Waishie kuangalia tu.

Ama kweli mwanzo mgumu,