Monday, July 6, 2015

MWANAMKE ALA MTOTO WAKE BAADA YA KUJIFUNGUA


Katika hali isiyokuwa ya kawaida mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la Li Zhenghua 24, amekutwa akifanya jaribio la kumla Mtoto wake aliyejifungua siku chache zilizopita, baada ya kumkuta taya yake ikiwa imenasa kuzunguka Mkono wa Mtoto wake.  
Majeraha ya mtoto baada ya kuliwa na mama yake

Tukio hilo la ajabu lilitokea katika Hospitali iliyoko Shenzhen Kusini mwa jimbo la Guangdong, China ambapo mwanamke huyo alifikishwa kujifungua na baadaye wahudumu wa Hospitali kufanya jitihada za kutafuta ndugu zake. 

Hata hivyo mwanamke huyo akiwa na siku ya tatu Hospitalini hapo alikutwa na nesi akiwa katika jaribio la kumng’ata mtoto ambapo madaktari walitumia nguvu na kufanikiwa kumuokoa mtoto huyo ambaye tayari alikuwa na jeraha mkononi.