Monday, October 5, 2015

NAPE: Kuondoka kwa Mzee Kingunge Chama kimepata ahueni

Chama cha Mapinduzi kimesema hatua ya kuondoka kwa Mzee Kingunge ndani ya CCM, imekuwa afadhali kwao kuliko angeendelea kubaki.

Katibu wa Itikadi na Uenezi amesema kuwa vitendo alivyokuwa anavifanya Mzee Kingunge vilikuwa vinawagawa wananchama ndani ya Chama

Nape amesema kuwa kitendo cha Mzee kingunge kumuunga mkono mgombea mmoja ndani ya Chama kilikuwa kinawagawa wanachama, alikuwa mzigo ndani ya chama.

Nape amesema kama chama walikuwa wanashindwa hatua gani wamchukulie mzee Kingunge.