JIJI LETU

Tuesday, December 1, 2015

TAARIFA MPYA YA KESI YA KAFULILA :::MAHAKAMA KUU KANDA YA TABORA YATUPILIA MBALI PINGAMIZI LA WAKILI WA HUSNA DHIDI YA KAFULILA.

Jana Mahakama Kuu Kanda ya Tabora inayosikiliza kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi jimbo la Kigoma Kusini ilofunguliwa na David Kafulila dhidi ya washtakiwa; Husna Mwilima, Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya uvinza kama msimamizi wa uchaguzi na Mwanasheria mkuu wa Serikali ilipokea pingamizi toka kwa wakili wa Husna Mwilima kutaka Mahakama Kuu isiendelee na kesi hiyo kwakuwa Mhe Kafulila hakufuata taratibu katika ufunguzi wa kesi hiyo.

Katika utetezi wa wakili wa Kafulila Daniel Lumenyera, Tundu Lissu waliomba mahakama itupilie mbali pingamizi hilo la wakili maarufu Fungamtama kwa hoja kuwa ni usumbufu kwa mteja wao na halina mana yoyote kwa kesi ya Msingi.


Leo Jaji anaesikiliza kesi hiyo Bi Leila amezingatia ombi la Fungamtama na utetezi Lumenyela na kuamua kutupilia mbali pingamizi hilo la wakili wa Husna na kumtaka Husna Mwilima kumlipa Kafulila gharama za usumbufu kwa kuweka mapingamizi yenye sura ya kupoteza muda na usumbufu.

leo Mahakama imendelea na hoja ya kutathimini gharama ya dhamana ambayo Mhe Kafulila atapaswa kuweka kama dhamana ya kesi ili kesi ya msingi iweze kuanza.

Uamuzi kuhusu kiasi gani Mhe Kafulila atalipwa kama dhamana utatolewa kesho na Mahakama.
at 10:40:00 PM
Newer Post Older Post Home

categories

AFYA AJALI AJIRA BIG BROTHER BONGO MOVIE Bongofleva Bongomovie BUNGENI ELIMU FASHION FIESTA FUMANIZI Habari Za Mitaani HIP HOP Instagram KIMATAIFA KITAIFA MAAJABU Madawa ya kulevya MAGAZETI MAPENZI MBELE MICHEZO RECORD SIASA TECHNOLOGY UDAKU UKATILI UTAFITI VITUKO WASANII WhatsApp Videos

Popular Posts

  • Magazeti ya Tanzania Septemba 20, 2015..
  • BAUNSA WA ZARI NA DIAMOND THE PLATNUMZ NI HATARI SIO KWA TIZI HILI
  • MAGAZETI YA LEO JUMATANO JULY 8 2015
  • KAMA HUKUBAHATIKA KUONA BASI HUU HAPA MKANDA MCHAFU WA ZARI THE BOSS LADY WA DIAMOND....CHEZEA INSTAGRAM WEWE
  • INASHANGAZA...AAMUA KUMN'GATA ULIMI MTU ALIYEMBAKA ILI KUPELEKA USHAHIDI POLISI.
  • Mimba ya Wema, Idriss apachikwa jina la Dk. Mwaka
  • Mama Afunguka Aunt Na Iyobo Kuachana!
  • Lowassa Aitikisa Nchi Wakati Wa Kutangaza Nia Ya Kugombea Urais....Bofya Hapa Kuona Picha
  • HUYU NDO KIJANA ALIYE MPIGA MPENZI WAKE BAADA YA KUBUSU KIFUA CHA DIAMOND
  • BAADA YA KUDAIWA KUWA KALIO LIMEPUKUTIKA, MODO CORAZON KWAMBOKA AWAKATA KIDOMO WAPAMBE KWA PICHA HIZI
Awesome Inc. theme. Powered by Blogger.