Saturday, January 23, 2016

KAULI NZITO ALIYOITOA BERNAD MEMBE KUHUSU KUFUTWA UCHAGUZI ZANZIBAR


Aliyekuwa waziri wa mambo ya nje amepinga uamuzi wa kufutwa matokeo yote Zanzibar na kusema dunia inashangaa na kuitaka CCM na serikali isiwaachie watu wawili tu kutafuta njia za kutatua mgogoro huo.
Membe anakuwa mwanasiasa wa kwanza mwandamizi kutoka chama tawala kuonesha waziwazi kutoridhishwa na uamuzi wa kufutwa kwa uchaguzi huo wa Rais wa Zanzibar, wawakilishi na madiwani ambao ulifanyika sambamba na uchaguzi wa Rais wa jamhuri wa Tanzania, wabunge na madiwani wa bara na visiwani.
Kinachoshangaza dunia si kuahirisha uchaguzi bali kufuta matokeo ya majimbo yote, alisema mwanadiplomasia huyo.