Kampuni hiyo imesema kuna uwezekano mkubwa kwa matokeo ya biashara yake kwa mwaka 2016 kuwa chini ya matarajio na kwamba haina matarajio tena ya kuwa na ukwasi kwa mwaka huu.
“Changamooto ya hali ya soko inayoathiri sehemu kubwa ya sekta ya usafiri wa anga barani Afrika, imekuwa ya muda mrefu zaidi ya uongozi ulivyotarajia awali,” taarifa ya Fastjet imeeleza.
Chanzo: Mwananchi