Meneja wa kampeni ya mgombea wa urais nchini Marekani kupitia tiketi ya chama cha Republican Donald Trump , ameshtakiwa kwa kumshambulia mwandishi wa habari katika mkutano wa kampeni.
Bwana Corey Lewandowski ameshtakiwa kwa shambulio dhidi ya aliyekuwa mwandishi wa Breitbart Michelle Fields.
Mnamo tarehe 8 mwezi Machi Bwana Lewandowski alimvuta na kumuangusha chini alipojaribu kuuliza swali na kujeruhiwa mkono.
Bwana Lewandowski anapanga kukana shtaka hilo,ilisema timu ya kampeni za bwana Trump