Saturday, April 2, 2016

EXCLUSIVE: Picha 5 Za Ujenzi Wa Kisasa Unaoendelea Uwanja Wa Ndege Dar, Jengo Jipya Litavyokuwa (Terminal 3 )

March 31 2016 millardayo.com ilipata kibali cha kupiga picha ujenzi unaoendelea wa kupanua uwanja na kujenga jengo jipya kwenye uwanja wa ndege Dar es salaam, naambiwa huu uwanja unategemewa kukamilika December 2017 na sasa hivi ujenzi wa umekamilika kwa asilimia 60, uniachie na comment yako hapa chini baada ya kutazama hizi picha mtu wa nguvu
DSC_0232
Huu ni muonekano wake wa nje kwa sasa ujenzi ukiwa unaendelea
Dar es Salam exterior july 2013 0012
Ujenzi ukikamilika 2017 huu ndio utakuwa muonekano wake wa nje
DSC_0129
Muonekano wake kwa karibu sehemu watakapokuwa wanaingilia abiria wanaosafiri
Dar es Salam exterior july 2013 0013
Ujenzi ukikamilika 2017 huu ndio utakuwa muonekano wake wa nje
DSC_0136
Hii ni sehemu watakapokuwa wanakaa abiria, ujenzi unaendelea.
Dar es Salam interior july 2013 Concourse
Ujenzi ukikamilika patakuwa hivi sehemu wanapopumzikia abiria
Dar es Salam interior nov 20123 Checking Hall
Uwanja mpya pia utakuwa na ngazi za umeme na za kawaida ujenzi ukikamilika
Dar es Salam exterior july 2013 0014
Kutakuwa kuna madaraja ambapo ndege inaegeshwa halafu abiria wanashuka au kupanda moja kwa moja na sio kushuka kwenye ngazi zinazobebwa na magari kama zamani
DSC_0189
Hili ndio daraja ambapo ndege mbili zinaweza kupark ubavuni kwa mara moja kupandisha abiria au kushusha.
DSC_0170
Muonekano wa daraja hilo kwa ndani, abiria akiwa anasubiria kuelekea kwenye ndege.
Dar Es Salaam Ph2 high-rev
Ujenzi ukikamilika huu ndio utakuwa muonekano wa uwanja huo kwa juu
-millard ayo