Sunday, May 29, 2016

Good News Kwa Muziki Wa Afrika Chriss Brown Kampost Wizkid Na Kuandika Hivi

Najua jina la Chriss Brown sio geni masikioni mwa watu wanaopenda muziki, basi leo May 29 2016 huenda ikawa ni good news kwa muziki wa Afrika, baada ya msanii kutoka Marekani Chriss Brown kumpost msanii Wizkid kutoka Nigeria.

Katika ukurasa wake wa Instagram Chriss Brown amempost Wizkid na kuandika maneno machache sana, lakini yanatafsirika kama kumualika mkali huyo wa Nigeria katika tour yake ya One Hell Of Nite Tour kwa mwaka 2016 atakayoifanya bara la Ulaya katika nchi za Uholanzi, Ujerumani na Denmark.


Muda mchache baada ya Chriss Brown kupost picha ya Wizkid, staa huyo kutokea Nigeria alipost nae picha kama hiyo na kuthibitisha kuwa kuanzia June 5 hadi June 11 2016 atakuwa katika Tour pamoja na Chriss Brown.