Sunday, June 19, 2016

Dakika 90 za Mchezo wa Mpira Zinanichosha - Wema Sepetu

Muigizaji Wema Sepetu, amesema mchezo wa soka unamchosha kuangalia kwa kuwa unatumia muda mrefu wa dakika 90 huku wachezaji wake wakihangaika mno kutafuta mabao tofauti na mpira wa kikapu (Basketball).

Wema anasema mara nyingi akiwa nyumbani kwake hupenda kuangalia mpira wa kikapu kwani hauchoshi na wachezaji huwa wanatumia muda mfupi kupachia mabao.
Ili aangalie soka na kumaliza muda wote wa mchezo ni lazima awe na kampani yake na mara nyingi iwe laivu uwanjani