Thursday, May 22, 2014

PENNY AKANUSHA UVUMI KUHUSU MAHUSIANO MAPYA YA KIMAPENZI BAADA YADIAMOND..SHUKA NAYO!!

Baada ya kuachana na Diamond Platnumz, Peniel  Mwingila aka Vj Penny ameendelea mbele na  maisha yake, lakini amekanusha kuwa na mpenzi mpya kama ambavyo wengi wamekuwa wakidhani hasa wanapomuona yuko karibu na mwanaume mwingine.

Leo Penny ameamua kuvunja ukimya wake na kukanusha habari zilizoenezwa katika mitandao ya kijamii kuwa ana mpenzi mpya aitwaye Rummy, hiki ndicho alichokiandika: “Ah come on people!!?? Kweli mi ni mkimya ila  sasa mnavuka mipaka, seriously?? Am so disappointed to see posts that Rummy is my new  boyfriend..mnatoa wapi hizi rumours? 

Just  because sijibu shutuma natupiwaga haimanishi mimi sio binadamu kila siku mnanizushia mapya  its not funny maisha yangu kutwa mnayafanya uwanja wa kutunga kitu, yes mnatukana na hakuna tusi jipya nawaacha ili mjifurahishe but  now u r crossing the line, I have alot of respect  for Rummy he is my homeboy na marafiki pia wa kiume nisiwe nao? Wengi wanajua rummy ni nani  yangu ila making these stories aint cool at all.

Enough has a limit! Nitukaneni all u want ila msinisingizie vitu sijafanya its just not fair at all.  Kama new boyfriend ntaweka mwenyewe mapenzi  hayajifichi ila tusizushiane uongo, nayavumilia  mengi ila hili too much.”