Saturday, September 20, 2014

BAADA YA KIMYA CHA MUDA MREFU:SAGUDA(MUME WA MAREHEMU RECHO) AKABIDHI MALI ZA RECHO UKWENI…

ALIYEKUWA mchumba wa marehemu Rachel Haule ‘Recho’, George Saguda amesema ameamua kupeleka mali zote za marehemu kwa ndugu zake ili wao wajue utaratibu wa kuzitumia.
George Saguda akiwa na aliekuwa mchumba wake marehemu Rachel Haule ‘Recho’
George Saguda akiwa na aliyekuwa mchumba wake marehemu Rachel Haule ‘Recho’
Akizungumza na paparazi wetu, Saguda alisema kwa sasa hahusiki na suala la mirathi ya Recho japo alikuwa akiishi na marehemu kama mke wake na kudai kuwa mali zote zilizokuwa zinamhusu Recho, tayari amezikabidhi kwa ndugu zake.
“Marehemu Recho nilikuwa nikiishi naye kama mke wangu lakini mali zake zote nimeshazikabidhi kwa ndugu zake kwa sababu wao ndiyo wanaohusika na suala zima la mirathi endapo kutakuwa na ulazima wa kunishirikisha basi wataniambia,” alisema Saguda.