Yapo madai kwamba, Mchungaji Christopher ambaye ni msaidizi wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God ‘TAG’, Kinondoni jijini Dar amekuwa akikerwa na tabia chafu anazozisikia za msanii Lulu Mathias Semagongo ‘Antu Lulu’.
Utashangaa sana kwamba, hayo yalisemwa na Anti Lulu mwenyewe juzi alipozungumza na gazeti hili kuhusu maisha anayoishi kwa sasa.
Lulu alisema: “Jamani, kama ni kubadilika najitahidi. Hata Mchungaji Christopher wa TAG, Kinondoni kwa Mchungaji Swai amekuwa akiniambia nirudi kanisani akaniombee.
‘
Antu Lulu’ akipozi.
Unajua yule ndiye aliyenilea kiroho nikiwa nasoma Sunday School pale, sasa anaposoma habari zangu anaumia, lakini sasa nimebadilika sana.”