Sunday, October 19, 2014

DAVIDO AWAGOMBANISHA CLOUDS FM NA TIMES FM..SOMA ZAIDI

Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, Dar es
Salaam imemzuia msanii kutoka Nigeria, Adedeji
Adelek ‘Davido’ kuperform katika tamasha la Fiesta
leo October 18, 2014.
Amri hiyo imetolewa jana kufuatia maombi ya
dharura yaliyowasilishwa mahakamani hapo na
Times Fm Radio waliopeleka maombi ya dharura
mahakamani hapo wakiitaka mahakama kumzuia
msanii huyo kuperform katika tamasha hilo, kwa
kuwa licha ya BASATA kukataa kutoa kibali cha
msanii huyo kwa maelezo kuwa tayari alikuwa
ameshachukuliwa kibali cha kuperform nchini
November 1 kwenye tamasha lililoandaliwa na
Times Fm Radio, Clouds Fm waliendelea na taratibu
zote bila kujali zuio hilo la BASATA.
Times FM pia wameomba Mahakama iamrishe
kulipwa fidia ya gharama na usumbufu
waliosababishiwa na walalamikiwa kadiri Mahakama
inafaa