Thursday, October 9, 2014

VIDEO:BIG BROTHER 2014 VITUKO VYAENDELEA , MMOJA AMTAKA MWENZIE AVUE NGUO ZOTE AMUONE ALIVYOUMBIKA



Mambo  yanazidi  kuwa  mambo  ndani  ya  jumba  la  "kikubwa"  la  Big  Brother  House  ambapo mwaka  huu   mashindano  hayo yamepewa  jina la  Hotshots( Big Brother Hotshots)
Baada  ya juzi  kamera  za  jumba  hilo  kuwanasa  washiriki  wa  Nigeria  na  Namibia  wakichezeana  makalio  yao, jana  Kamera  hizo  ziliwadaka  Tayo(Nigeria)   na  Ellah (Uganda)  wakipigana  "Sound"
Katika  video  iliyopachikwa  hapo  chini, Mshiriki  wa  kiume  wa  Nigeria  anasikika  akimshawishi  Mshiriki  wa  kike  wa  Uganda  akubali  kuvua  nguo  na  kuoga  mbele  yake  ili  amshuhudie  alivyoumbika.....
Kudhihirisha  kwamba mshikaji  yuko  "deep"  katika  sekta  ya  mahaba, Sauti  laini  yenye  tabasam  la  kimahaba  inasikika  ikimpasha  mrembo  huyo  wa  Uganda  kuwa  yeye  ni  mzuri  kuliko  washiriki  wote  wa  kike  walioko  ndani  ya  jumba  hilo  na  kwamba  endapo  atakubali kuvua  jamaa  atafurahi  sana!


 Big Brother Africa