JANA katika ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem, jijini Dar, wasanii kibao wamedondosha bonge la shoo katika Usiku wa Uswazi na Waswazi, shoo iliyoandaliwa na Defatality Music ikiwashirikisha mastaa wakongwe kama Chid Benz, Top in Dar ‘TID’ ,Yakuza Mobb, Kalapina, aka “Mbuge Mtarajiwa’’, Pam D pamoja na wasanii kibao wanaokuja kwa kasi wakiwemo Kundi la Umeme na Wabibi.
Wasanii wengine waliodondosha burudani ni pamoja na Kala Pina aka ‘’Mbunge mtarajiwa’’ Top in Dar ‘TID’, Kundi la Umeme, Inspector Haroun, Yakuza Mobb, Mesen Selekta, Pam D na wengine kibao.