Thursday, January 1, 2015

"...NILIACHA SHULE KWA SABABU YAKE.." SOMA MKASA HUU WA BINTI MDOGO WA CHUOKIKUU TAFADHALI!


Mimi ni binti wa miaka 23, ninaishi na 
wazazi wangu wote wawili, ni mtoto wa pili 
kuzaliwa kwenye familia yetu. Nilianza 
mahusiano ya kimapenzi nikiwa chuoni 
mwaka wangu wa kwanza na kijana mmoja 
aitwaye Erick, Nilitokea kumpenda sana 
kwani alikuwa ndio mwanaume wangu wa 
kwanza. Kwetu walimjua na hata kwao pia 
nilifahamika.Nilikuwa na Erick mpaka 
nilipofikamwaka wa pili hapo chuoni 
Ambapo sasa tuliamua kukodi chumba 
kimoja na kuishi wote. Katika kipindi hichi 
niliona tabia za Erick hazieleweki anaweza 
kurudi usiku sana akiwa hajitambui na hata 
kulala tu chini mpaka asubuhi. Nilikuwa 
nikimshauri lakini alikuwa ni mgumu sana 
kunielewa.Siku moja alirudi akiwa mzima 
majira ya saa kumi jioni hivi, kamasikosei 
ilikuwa ni siku ya ijumaa, tena mimi nilikuwa 
ndio natoka kwenye kipindi.Alikuja siku hiyo 
akiwa na furaha sana huku akiwa na chupa 
mbili moja ya wine na nyingine ya amarula, 
Alizifungua zote nakuanza kunywa huku 
tukipiga story na kucheka, na mimi 
kwasababu pia nilikuwa nakunywa alini 
miminia natukawatunakunywa wote, Nilipo 
anza kulewa alianza kunishawishi nivute 
sigara ambayo yeye alishaiwasha nakuanza 
kuivuta bila kusita nilichukua sigara na 
kuivuta kwakuwa nilimuamini sana 
Erick.Muda si mrefu nilipata usingizi wa 
ajabu ambao ulinifanya nisitambue 
chochote kilichoendelea pale.Kesho yake 
majira ya saa tano Asubuhi nilipata fahamu 
na kuamka, nilimuuliza Erick kilichotokea 
lakini hakunipa jibu lililo eleweka sikuwa na 
raha kabisa kwani nilitamani kupata ileraha 
tena, Nilishawishika kumuuliza erick kuhusu 
ile sigara.na yeye hakunijibu ila alinipa tu 
myingine akasema vuta hii hapa.Huu ndio 
ulikuwa mwanzo wa kuharibu masomo 
yangu. Kumbe kipindi chote Erick alikuwa 
anatumia madawa ya kulevya akichanganya 
kwenye sigara, na akaona haitosha anipe na 
mimi.Basi na mimi niliendelea na tabia hiyo 
hadi darasani nikawa siendi tena walimu 
walikuwa wananiulizia sana kwani nilikuwa 
kati ya wanafunzi wazuri sana darasani. 
Niliendelea na tabia hiyo hadi wazazi wangu 
walipokuja kujua na kunipeleka kwenye 
kituo cha waathirika wa madawa. Kipindi 
hicho Erick alikuwa amechanganyikiwa 
kabisa kwa madawa na chuo alisha acha 
yuko tu kwao.Nilikaa huko kwenye kituo 
hicho kwa muda wa miezi sita, nikiwa 
napata ushauri pamoja na dawa za 
kupunguza hamu ya madawa ya kulevya. 
Nashukuru sasa hivi niko nyumbani na 
ninaendelea vizuri.NAWASHAURI WANAVYUO 
WAJARIBU SANA KUEPUKA VISHAWISHI 
VINAVYOWEZA KUHARIBU MAISHA YAO KWA 
UJUMLA!