Saturday, January 3, 2015

UPAJA WA JACK WA MAISHA PLUS WAZUA UTATA!

 
MAPAJA ya staa wa Shindano la Maisha Plus Season 2, Jacqueline Dustan ‘Jack Maisha Plus’(Pichani juu) yamezua tafrani baada ya wanaume wakware kumsimamia na kumshangaa kutokana na kuvaa nguo fupi iliyomuacha mtupu mapajani.Kwa mujibu wa chanzo, tukio hilolililowafanya watu washindwe kuendelea na shughuli zao kwa muda lilitokea juzikati katika mgahawa maarufu wa Cape Town Fish Market uliopo Msasani jijini Dar ambapo staa huyo alipoona watu wanazidi kumkodolea macho, aliamua kutimka. 
“Nilikwenda na kustarehe na marafiki zangu ambao nilikuwa siko nao muda mrefu hapa nchini, sasa nikashangaa ghafla watu wamenizunguka wanahangaikahangaika hadi shughuli za watu hotelini hapo zikawa haziendi vizuri, nikatoka nduki,” alisema Jack.