Friday, May 22, 2015

VIDEO:WALEMAVU WAANDAMANA NA KUFUNGA BARABARA JIJINI DAR

Walemavu wakiwa wamekaa barabarani wakati wa maandamano hayo.
Wananchi wakitaharuki kufuatia maandamano ya walemavu kuelekea kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Hali ilikuwa tete.
Jeshi la Polisi wakihakikisha ulinzi na usalama wakati wa maandamano hayo.
Maandamano yakishika kasi.
Baadhi ya walemavu wakihojiwa na waandishi wa habari.
Foleni ya magari iliyosababishwa na maandamano ya walemavu.
Sintofahamu na taharuki juu ya maandamano hayo.
...baadhi wamekaa barabarani na wengine wamesimama.
...hivi ndivyo hali halisi ilivyokuwa.
...wakikaa barabarani kuzuia magari yasipite.
...wananchi wakizidi kushangaa hali hiyo.
WALEMAVU jijini Dar es Salaam leo wameandamana kwenda Ofisi za Mkuu wa Mkoa zilizopo Ilala jijini Dar na kufunga barabara za Kawawa na Uhuru wakilalamikia kuvunjwa kwa meza zao za biashara zilizopo eneo la Karume.
Maandamano hayo yalisababisha msongamano mkubwa wa magari na kupelekea usumbufu mkubwa kwa abiria na madereva waliokuwa wanatumia barabara hizo.