Thursday, July 9, 2015

AMA KWELI KENYA SIO WENZETU ...WALETA TRENI HII YA KISASA...SISI BADO NA MABEHEWA MABOVU





HONGERENI KENYA, NDEGE TAKRIBANI 100, RELI MPYA NA TRENI YA KISASA!
Ndugu zangu,
Kenya wanazidi kupiga hatua, tena hatua za maana sana. Sina maneno ya kuongeza kwa sababu picha zinaongea. Tanzania ina kila kitu cha kujifunza Kenya,
Sisi Tanzania tuna vivuti vya utalii vingi mara 10 ya Kenya, lakini Kenya inapata fedha za utalii mara 5 kutushinda.

Sisi hatuna hata ka-ndege ka "kimagumashi", wenzetu Shirika lao linazidi kuimarika na kupambana na mashirika makubwa duniani.
Nadhani lazima tutafakari kama kweli uongozi wa nchi yetu umetutendea haki kwa miaka 50 sasa. Tuchukue hatua, ama tuache kulalamika.
J. Mtatiro,
DSM