Yafuatayo ni mambo sita ambayo yametoka kwenye kauli ya Polisi Kilimanjaro kupitia kwa kamanda wake Felgensi Ngonyani mbele ya Waandishi wa habari leo August 14 2015.
1. Tarehe 13 August 2015 Usangi wilaya ya Mwanga, katika mazishi yale kulikua na taarifa mbalimbali kwamba viongozi mbaimbali wangehudhuria akiwemo Rais Jakaya Kikwete na baadae tulipata tetesi kwamba na Edward Lowassa naye angehudhuria.
2. Kweli siku husika tukapata taarifa za msafara wa Edward Lowassa ulipopita Mwanga mjini, nikapata taarifa kutoka kwa mkuu wa Upelelezi Mwanga kwamba msafara wa Lowassa ukiwa na magari zaidi ya 70 na pikipiki zaidi 600 wanataka kuja kwenye msiba, mimi nilikua kwenye msiba na nikaona wingi huo wa magari na pikipiki kusingepatikana sehemu ya maegesho.
4.Baada ya kuwapa taarifa hiyo wale viongozi walikataa kwa kusema hawawezi kwenda peke yao bia Wafuasi wao, wakaamua warudi walikotoka.
5. Baadae kukawa na taarifa kwenye mitandao kwamba nimeongea na Waandishi kwamba kuzuiwa kwa msafara ule kulitokana na shinikizo la viongozi wa ngazi ya juu na kwamba Polisi tunaonewa ile sio matashi yetu, hiyo ni uzushi na sikuongea jana na Waandishi wahabari.