Wednesday, October 14, 2015

LOWASSA ASEMA KURUDISHA KATIBA YA WANANCHI

Watanzania wametakiwa kuhakikisha wanamchagua kwa kura nyingi zaidi mgombea wa urais Edwrad Lowassa, kwani serikali itakayoundwa chini ya umoja huo itahakikisha inarejesha katiba ya wananchi.
Wakati joto la uchaguzi likizidi kupanda nchini, Freeman Mbowe ni mwenyekiti wa Chadema taifa
Aidha amewahakikishia watanzania kuwa kwa mara ya kwanza hakuna kura hata moja itakayoibiwa na CCM, huku akiwataka kuhakikisha wanalinda kula kikamilifu.
Hayo yanajili ikiwa ni miaka 54 sasa Tanzania ikiwa chini ya utawala wa chama kinachotajwa kuchokwa na watanzania cha CCM.
Akiwa bado ndani ya kanda ya ziwa, mgombea wa urais Edward Lowassa ameendelea kupata mapokezi ya kifalme ambapo hii leo amehutubia mikutano mikubwa minne katika majimbo ya Ngara mjini, na vijiini, Bilaharamuro kabla ya kuhimisha kwa kishindo katika uwanja wa maswimbwe mjini Mbogwe,
 
Mgombea huyo wa urais Edward Lowassa na timu yake ya kampeni anatarajiwa kuhitimisha kampeni zake kanda ya ziwa kwa kuhitimisha kwa wilaya zote zilizoko ndani ya jiji la Mwanza.