JIJI LETU

Monday, November 30, 2015

HIVI UMELISIKIA HILI LA KUKAMATWA KWA MABUNDA YA NOTI YAKIWA KWENYE NDOO,BASI HII NDIYO TARIFA SAHIHI.


Habari zilizosambaa mitandaoni kuhusiana na mabunda ya noti za dola ya Kimarekani kuwa zimekutwa nyumbani kwa mmoja wa watuhumiwa wa mtandao wa wizi bandarini na TRA sio za kweli, Globu ya Jamii inaweza kuthibitisha.Ukweli ni kwamba mabunda hayo ya noti yalikamatwa huko jijini York, Portland, Marekani Mwezi Septemba mwaka 2010, na sio hapa Dar es salaam, Tanzania kama ambavyo wadau wengi wa mitandao hasa ya Whatsapp na Instagram wanavyovumisha.

Tumelazimika kutoa habari hii ili kuokoa wadau wetu wengi katika vuguvugu hili la uvumi wa mitandaoni ambayo hupelekea kazi kuwa ngumu kwa wengi wetu tunaotafuta na kutoa taarifa za uhakika na ukweli. Maana samaki mmoja akioza wote huonekana wameoza.


Vile vile hii ni kuwafumbua wale wote wanaohusika kusimamia na kutekeleza sheria ya mitandao wawe macho na kuanza kuchukua hatua madhubuti ili kupunguza kama si kuondoa kabisa tabia hii mbaya ya kusema uwongo kila kukicha.
at 8:40:00 AM
Newer Post Older Post Home

categories

AFYA AJALI AJIRA BIG BROTHER BONGO MOVIE Bongofleva Bongomovie BUNGENI ELIMU FASHION FIESTA FUMANIZI Habari Za Mitaani HIP HOP Instagram KIMATAIFA KITAIFA MAAJABU Madawa ya kulevya MAGAZETI MAPENZI MBELE MICHEZO RECORD SIASA TECHNOLOGY UDAKU UKATILI UTAFITI VITUKO WASANII WhatsApp Videos

Popular Posts

  • EXCLUSIVEE...AUNTY EZEKIEL AJIFUNGUA MTOTO WA KIKE
  • Mwanafunzi aliye kuwa 'kichwa' darasani apata 0 kwenye mtihani wa mwisho, Imezua gumzo mtandaoni!
  • Muziki wa Tanzania wazidi kung’ara, Vanessa, Diamond na Shaa washika chart kubwa za kimataifa
  • KURASA ZA MWANZO NA MWISHO ZA MAGAZETI YA LEO JUNE 30,2014
  • FILAMU MPYA YA MANAIKI YAITIKISA NCHI, WASANII KIBAO WAHUSIKA!!!!!, WACHEKI HAPA
  • Picha: Filamu ya ‘Mbwa Mwitu’ ya Kajala yazinduliwa Mlimani City..!! FANYA KUONA TRELA HAPA NA PICHA ..!!!
  • Aishi siku 555 bila moyo wake, akitumia moyo feki kwenye begi
  • Maajabu ya Paka Mwizi wa Nguo za Ndani
  • KAMA HUKUBAHATIKA KUONA BASI HUU HAPA MKANDA MCHAFU WA ZARI THE BOSS LADY WA DIAMOND....CHEZEA INSTAGRAM WEWE
  • SHUHUDIA KIPINDI AMBACHO KAJALA YUPO HOTI NA MVUTO ZAIDI
Awesome Inc. theme. Powered by Blogger.