Thursday, February 11, 2016

Ajali ya basi na lori yaua Tanga


WATU kadhaa wanahofiwa kufariki dunia wakiwemo madereva wawili baada ya basi la abiria la Simba Mtoto lililokuwa linakuja jijini Dar es Salaam kupata ajali kwa kugongana na lori katika kijiji cha Pangamlima, Barabara ya Tanga-Segera mkoani Tanga leo asubuhi.
Tovuti hii imeongea na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga ambaye amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza kuwa zoezi la uokoaji bado linaendelea hivyo likimamilika atatoa taarifa rasmi kuhusu ajali hiyo.