Sauti Sol kwa sasa wanatamba na wimbo wao wa ‘Unconditionally Bae’ Ft Ali Kiba ambayo kwa sasa inawatazamaji 569,000 ndani ya siku 11, kundi hili limepata baraka nyingine kubwa huko kwao Kenya.
Sauti Sol wametajwa kuwa “Billboard Africa’s Most Promising Music Group, na The Standard Newspaper 2016 Agenda Setters and DRUM Magazine East Africa’s 2015 Movers and Shakers”
Wiki hii Sauti Sol wamebarikiwa na kitu ambacho wasanii wengi wanataka Kenya ambacho ni kuwa na picha zao kwenye gari ya matatu.