Thursday, May 5, 2016

Urusi Sasa Kujikita Tanzania, Yapanga Kujenga Mtambo wa Nyuklia Tanzania

Makampuni makubwa ya Viwanda na uzalishaji ya Kirusi ya "Russian Helicopters", "United Aircraft Corporation (UAC)" na "United Wagon Company (UWC)" yako tayari kuwekeza kwenye miradi ya viwanda nchini Tanzania.

Waziri wa viwanda wa Urusi amesema Urusi iko tayari kujenga nuclear reactor nchini Tanzania kwa ajili ya tafiti na kwa ajili ya mambo ya afya.

Huu ni mpango wa Urusi kufufua uhusiano wake na nchi za Afrika kwa upya tangu miaka ya 90 kwa kupitia mshirika wake wa zamani, Tanzania.