Wednesday, September 24, 2014

AMBER ROSE ASHAMBULIWA KWA PICHA ALIZOSAMBAZA, AMEJISAHAU NI MKE WA MTU – MASHABIKI (18+)

Amber Rose 1Huwa haichukui muda mashabiki kushambulia mastaa mbalimbali hasa wanapoona kwamba wanavuka mipaka na kuharibu maadili au kuendeleza vitu ambavyo vinawatafutia umaarufu kwa njia mbaya.
Mdau mmoja mkubwa wa muziki duniani alipokuja Afrika aliwahi kuwaambia Watangazaji wa Radio ni kiasi gani ambavyo mastaa wa dunia wamekua wakilipwa pesa nyingi kupiga picha wakiwa watupu na kuzifanyia biashara kwa kuziuza mamilioni ya pesa kwenye Majarida pamoja na vyombo vingine vya habari.
Yani biashara imegeukia huko na akamtolea mfano Rihanna ambae aliwahi kupiga picha za namna hii na kulipwa mamilioni ya fedha za Kitanzania kwa sababu tu ya picha zake 7 za utupu zilizotumiwa.
Amber Rose 2Katika siku za karibuni taarifa kubwa ambazo zimetangazwa mpaka na vyombo vikubwa vya habari duniani ni kuhusu tatizo la kuvujishwa kwa picha za utupu za watu maarufu wakiwemo Waigizaji wa dunia kama Meagan Good na Gabrielle Union ambae alikuwepo Tanzania siku kadhaa zilizopita.
Amber Rose 3Mashabiki mbalimbali na watumiaji wa mitandao wamemshambulia Amber Rose na kusema kwa sasa mama huyu wa mtoto mmoja aliepata na rapper staa Wiz Khalifa ameshakua kiumri na tayari ni mke wa mtu hivyo haya mambo awaachie wenye ulimbukeni wa umaarufu na pesa za haraka zinazoambatana na kashfa.
Kibaya zaidi kilichofanya wengi wamlaumu ni baada ya kujulikana kwamba picha hizi alizisambaza kwa makusudi na sio kama kisingizio cha wengine kwamba wamepoteza simu au kuibiwa.
Amber Rose 4
Amber Rose 5