Saturday, September 6, 2014

MSANII HUYU WA VICHEKESHO AFARIKI DUNIA..!!

Enzi za uhai wake Joan Rivers
Mchekeshaji maarufu nchini Marekani Joan Rivers amefariki dunia akiwa na umri wa miaka themanini na na mmoja.
Joan alikua amelazwa katika hospitali moja mjini New York kwa wiki kadhaa sasa akisumbuliwa na maradhi ya moyo.
Melissa binti wa Joan,Akitangaza juu ya kifo cha mamake alimuelezea mama yake kua maishani mwake alikua akipenda kuona watu wana tabasamu usoni ama vicheko.
Joan River alianza shughuli zake za ucheshi kama muigizaji wa kawaida tu nusu karne iliyopita, na anatajwa kua mwanamke maarufu na bora katika ucheshi jukwaani.

BBC