Tuesday, October 14, 2014

AJALI MBAYA YA BASI LA HAPPY NATION NA GARI DOGO....MFANYAKAZI WA BENKI NA WATU WENGINE WATATU WAFARIKI DUNIA


Wafanyakazi wa Benki moja hapa nchini wamekumbwa na simanzi iliyosababishwa na kifo cha mwajiriwa mwenzao kilichotokana na ajali iliyotokea jana jioni huko Hedaru, Wilayani Same mkoani Kilimanjaro iliyohusisha gari lenye namba za usajili T653 BZR na basi la Happy Nation.
 
Imeripotiwa kuwa watu wote wanne waliokuwemo ndani ya gari dogo walipoteza uhai papo hapo.
 
Picha zilizopachikwa hapo chini zinaonesha jinsi gari hilo dogo lilivyoharibika vibaya baada ya ajali.