Thursday, October 16, 2014

BIG BROTHER AFRICA: MSHIRIKI WA KIKE WA BOTSWANA AJILEGEZA KWA JEMBE LETU LA KIUME ( IDRIS) LINALOIWAKILISHA TANZANIA


Siku washiriki wa BBA Hotshots wanatambulishwa, mwakilishi wa Tanzania, Idris Sultan alimwambia mtangazaji IK kuwa cheche zake zipo kwenye masuala ya wanawake. Huenda sasa shughuli imeanza.

Baada  ya  binti  mrembo  wa  Botswana( Goitse)  kumzingua  mshikaji ( Idris ) aliyekuwa  ametupa  jiwe kumtaka  awe  mpenzi  wake, hatimaye  Idris  jana alimnasa binti  huyo na kula  naye  dinner pamoja...
 
Ni  kama  ndoto  vile!!....Dinner  hiyo  iliandaliwa  na  kufanikishwa  na  washikaji  zake  wa  karibu  Nhlanhla na JJ  ambao  walisaidia kupika chakula hicho  kuhakikisha kuwa wawili hao wanakuwa na mtoko   utakaowafurahisha.
 
Wakati wote wa dinner, Ellah, Sabina, M’am Bea na Luis walishiriki sehemu yao ya kuwahudumia chakula. Idris alimuuliza Goitse maswali kutaka kumfahamu zaidi na kumuuliza kama anaamini katika uhusiano wa mbali, long-distance relationships. Goitse, hata hivyo alionesha kuvutiwa zaidi na urafiki  tu  kuliko mapenzi.
 
Matukio  yote  ya  Big Brother  yako  hewani  kupitia  site  yako  pendwa  ya  www.bigbrotherafricans.com

Usikubali  kupitwa  na  tukio  lolote....Video  zote, picha  za  washiriki  na  live  updates  mbalimbali  zinaruka  masaa  24  kwa  siku  zote  63  za  shindano  hili. 

Unataka  kushuhudia  kila  kitu??  << BOFYA  HAPA>>

Ingia  hapo  juu  kwa  matukio  ya  moja  kwa  moja  toka  ndani  ya  jumba  la  big  brother  africa.
-Via mpekuzi