Friday, October 3, 2014

JUZI WEMA SEPETU ALITIMIZA MIAKA 26.....LEO DIAMOND PLATUNUMZ KATIMIZA MIAKA 25.... ANATAKA ATOE KADI KWA WATU WATANO TU



Leo, Octoba 2,  Staa wa muziki wa Bongo Flava Nasibu Abdul 'Diamond Platunumz' anasherehekea siku yake ya kuzaliwa akiwa anatimiza umri wa miaka 25.

Mpenzi wake, Wema  Sepetu ambaye wengi wanasubiri kusikia atasema nini au atatoa zawadi gani kwa Diamond ambaye alimpa gari aina ya Nissan Murano, ameandika machache kwenye Instagram na kueleza kuwa anajipanga kuandika ujumbe mzuri zaidi.

“Happy Birthday to you my original soul... ngoja nitulie kwanza ndo niandike caption maana nina mengi kwa kweli... ila jua nakupenda sana...”Ameandika Wema.
  
Naye Shetta ameamua kumlipa fadhira ya shukurani Diamond Platinumz kwa mchango wake kwenye maendeleo ya muziki wake ikiwa ni sehemu ya kumtakia heri ya siku ya kuzaliwa.

diamond nae facebook awakaribisha mashabiki zake hivi....
"Najua wote tungependa tufurahie kwa pamoja siku yangu hii ya kuzaliwa, lakini kwa bahati mbaya hakuna ukumbi utaoweza kututosheleza... sasa tafadhali naomba niambie, unahisi ni kwanini nikupatie wewe kadi hii ili uwe muwakilishi wa Mashabiki zangu??? (nataka nitoe kadi kwa watu 5)......

(i know all of you guys would love to celebrate my birthday with me tonight, bt unfortunately due to lack of the venue we won't be able to... so please tell me why should i give you this invitation Card to represent my all fans around the World...?)"


Photo: Najua wote tungependa tufurahie kwa pamoja siku yangu hii ya kuzaliwa, lakini kwa bahati mbaya hakuna ukumbi utaoweza kututosheleza... sasa tafadhali naomba niambie, unahisi ni kwanini nikupatie wewe kadi hii ili uwe muwakilishi wa Mashabiki zangu??? (nataka nitoe kadi kwa watu 5)......  (i know all of you guys would love to celebrate my birthday with me tonight, bt unfortunately due to lack of the venue we won't be able to... so please tell me why should i give you this invitation Card to represent my all fans around the World...?)