Sunday, December 21, 2014

MAUAJI YA WATOTO 8 AUSTRALIA, MAMA MZAZI ASHITAKIWA

Maua na midoli ikiwa jirani na nyumba yalipotokea mauaji hayo.
Mmoja wa ndugu wa marehemu akilia kwa simanzi.
Waombolezaji wakilia wakati wa ibada ya kuwakumbuka watoto hao leo asubuhi.
Watoto pia waliwakumbuka wenzao katika ibada hiyo.
Mamlaka nchini Australia imemfungulia mashitaka ya mauaji ya watoto nane, Mersane Warria (37) aliyewaua watoto 8, wanaye 7 na 1 mpwa wake, jijini Cairns juzi, Ijumaa!
Mama huyo ameshitakiwa akiwa hospitali ambapo anaendelea na matibabu akiwa chini ya ulinzi baada ya kujijeruhi na kisu baada ya kufanya mauaji hayo akiwa nyumbani kwake jijini Cains, Austarlia.
Uchunguzi bado unaendelea kugundua chanzo hasa cha mauaji ya watoto hao nane, wanne wakiume na wanne wa kike wakiwa na umri kati ya miezi 18 hadi miaka 14.
Polisi walikuta sialaha kadhaa ambazo bado zinaachunguzwa vikiwemo visu katika eneo la tukio.
Miili ya watoto hao iligunduliwa na mama mmoja aliyefika nyumbani hapo (juzi) Ijumaa asubuhi.
Ibada ya misa imefanyika leo asubuhi jijini Cairns kuwakumbuka watoto hao.