Thursday, December 11, 2014

Singa Singa wa IPTL, Harbinder Singh Sethi atoweka Nchini

Mmiliki wa kampuni ya IPTL,Harbinder Seth, ametoweka na vyombo vya usalama vimejiandaa kumkamata ndapo atarejea nchini, Raia mwema limeelezwa.Singh ambayekampuni yake ya Pan african Power solution (PAP) inadaiwa kununua umiliki wa kampuni ya kufua umeme ya IPTL katika mazingira yaliyozua utata, anadaiwa kuwa yupo nchini Kenya au Africa ya Kusini.

Gazeti hili limeelezwa kwamba Singh aliondoka nchini siku chache kabla ya bunge la Tanzania ya wahusika wote wa makosa ya kijinai katika suala hilo wakamatwe na hatua za kisheria dhidi yao zichukuliwe.
singa

Azimio namba moja la Bunge lilisema;….Takukuru, Jeshi la polisi na vyombo vingine husika vya Ulinzi na usalama viwachukule hatua stahiki za kisheria, kwa mujibu wa sheria za nchi yetu,watu wote waliotajwa na Taarifa maalumu ya kamati kuhusika na vitendo vyote vya kijinai kuhusiana na miamala ya akaunti ya Escrow, kuhusika katika vitendo hivyo vya jinai kufuatia uchunguzi mbalmbali unavyoendelea.

Raiamwema limeelezwa kwamba, singh ambaye katka siku za nyuma alikua akipenda kufika katika hotel mbalimbali ikiwemo Sea cliff ya Jijini dar es salaam, Sasa hayupo Dar es salaam lakini anafuatilia kea karibu yanayo endelea.

Naweza kukuthibitishia kwamba sethi hayupo nchini hivi sasa. Kwenye hili swala sitaki kuwa mzungumzaji wake lakini nafahamu kwamba aliondoka kabla ya Bunge kuazimia kwamba wahusika wakamatwe.

“Sasa kama alifanya akijua kwamba hayo hayo yanaweza kutokea mimi sijui. Siwezi pia kujibu swali lako la atakuja lini sabau sijaambiwa. Hata hili la kukuambia kwamba hayupo nimekwambia kwa sababu tunafahamiana na sitaki kukudanganya, Alisema mmoja wa watu wafanyakazi wa Sethi ambaye hata hivyo gazeti hili haliwezi kumtaja jina