Friday, December 26, 2014

UMEISIKIA HII YA WALIOTAKA KUIBA SANAMU LA BIKIRA MARIA KANISANI?

MarVijana watatu Songea wametakiwa kwenda na wazazi wao kutubu dhambi za kutaka kuiba sanamu la Bikira Maria katika Kanisa Katoliki la Kigango cha Samora.
Katekista wa Kigango hicho Keneth Mhagama walisema vijana hao walifanya jaribio hilo usiku wa manane baada ya ibada ya mkesha ambapo walinzi walifanikiwa kuwadhibiti kabla hawajafanikiwa na wakawekwa mbaroni.
Vijana hao ni Ahmed, Mohammed na Leonard ambapo Padri wa Kanisa hilo Cristom Kapinga amesema vijana hao wanatakiwa kutubu la sivyo watawaacha kwenye mikono ya sheria washughulikiwe.
Chanzo cha Habari: Gazeti MtanzaniaDecember 26.