Monday, February 9, 2015

DAVINA AMUONEA WIVU LULU

MSANII wa filamu Bongo, Halima Yahaya ‘Davina’ amejikuta akimuonea wivu msanii mwenzike, Elizabeth Michael ‘Lulu’ kutokana na kuwa chini ya uangalizi wa meneja na kulipwa pato kubwa kwenye filamu.
Msanii wa filamu Bongo, Halima Yahaya ‘Davina’.
Akipiga stori na paparazi wetu kuhusiana na ishu ya msanii huyo ambaye ni mdogo zaidi yake, kufikia hatua ya kulipwa shilingi milioni kumi na tano kwa filamu moja, ni mafanikio makubwa ambaye anayatamani sana.
“Yani hao wanaompinga Lulu wanamuonea wivu tu, naamini analipwa hiyo fedha sababu yupo chini ya usimamizi wa kampuni kubwa ya Proin Promosheni, natamani na mimi ningekuwa na meneja wangu ningenufaika zaidi kama yeye,” alisema Davina.