Monday, April 20, 2015

DIAMOND: SIITAJI JINSI YA MWANANGU

Musa Mateja
STAA wa Muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, amefunguka kuwa hayupo tayari kuitaja jinsi ya mtoto wake mtarajiwa kwa kuogopa wafitini.
Staa wa Muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Akizungumza na mwanahabari wetu, Diamond anayetarajia kupata mtoto kwa mpenzi wake wa sasa, Zarinah Hassan ‘Zari’, alisema anamshukuru Mungu hadi sasa tayari anaijua jinsi ya mwanaye lakini hayupo tayari kuitaja.“Tayari baby ameshapima na kujua jinsi ya mtoto lakini siwezi kuitaja kwa sasa maana wabaya nao ni wengi sana mjini hapa,” alisema Diamond.