Monday, April 20, 2015

WASTARA AWAHIMIZA MASTAA KUZAA

Staa wa filamu Bongo, Wastara Juma.
Gladness Mallya
STAA wa filamu Bongo, Wastara Juma amewahimiza mastaa wa kike kuzaa mapema na kuachana na tabia ya kutoa mimba hovyo.Akipiga stori na gazeti hili, Wastara alisema kutokana na maisha kuwa mafupi na kubadilika kila kukicha anawasihi mastaa wa kike kuzaa mapema na kuachana tabia ya kutoa mimba hovyo.
“Nawasihi mastaa kuachana na tabia ya kutoa mimba kwani hawajui Mungu amewaandikia watoto wangapi katika maisha yao, pia waache tabia ya kutoa mimba kwani baadaye wakati wakiwa tayari kuzaa watashindwa kuwapata na kujikuta wakijilaumu,” alisema Wastara.