Wednesday, April 15, 2015

TAMKO LA AL-SHABAB KUHUSU KUISHAMBULIA TANZANIA

Kundi la wapiganaji wa Al Shabaab.
Kutokana na uvumi uliosambaa kwenye baadhi ya vyombo vya habari vikiwemo vituo vya Redio, Televisheni, Magazeti na Mitandao ya kijamii kuhusu wapiganaji wa kikundi cha Al Shaabab cha Somalia kuishambulia nchi ya Tanzania kama walivyoishambulia Kenya na Somalia siku chache zilizopita.
Kiongozi wa kundi hilo ametoa tamko kuhusu taarifa hizo alipokuwa akihojiwa na kwenye kituo cha Radio ya YARAT FM ya Somalia jana Saa 2:00 asubuhi kwenye kipindi cha Makhal Twalib.
AKANUSHA
Kiongozi huyo alisema, "Al Shaabaab kamwe hawajawahi kufikiria kushambulia nchi ya Tanzania kwa kuwa hawana sababu ya kufanya hivo."

Alisema kwamba mbali ya kuzingatia kuwa, Tanzania ina raia wengi ambao ni waumini wa dini ya Kiislam lakini pia wanajua na kutambua msaada wa Mwalim Julius Kambarage Nyerere mwaka 1995 alipotoa msaada wa tani 500,000 za mahindi kipindi ambacho Somalia ilikumbwa na baa la njaa. Hivyo hawawezi kulipa unyama chuo kwa Marehemu Baba Wa taifa.

Pia kiongozi huyo aliongeza kuwa, Tanzania haijapeleka jeshi lake somalia yenyewe nchi kama nchi tofauti na Kenya na Uganda. Wanajeshi wachache watanzania walioko somalia ni katika jeshi la AU na sio kwa amri ya Serikali ya Tanzania.

AIPA POLE TANZANIA
Kiongozi huyo pia alitoa pole katika muda Wa siku mbili ambao watanzania hususani wanachuo waliokuwa katika hali ya sintofahamu na pia vyombo vya usalama ambavyo vililazimika kuimarisha ulinzi katika sehemu nyeti mbali mbali.

Kiongozi huyo kamaliza Kwa kusema kwamba wao wanazingatia msemo Wa Quran kwamba, “Fight those who fight you, spare those who don't fight you”
CHANZO: DJ SEK BLOG