Sunday, June 7, 2015

YAMOTO BAND WAFANYA KWELI ESCAPE ONE JIJINI DAR

Yamoto Band kazini.
Sehemu ya mashabiki wakijimwaya.
Hawa nao wakioneshana maujuzi.
Tundaman akikamua baada ya kuachiwa jukwaa na Yamoto Band.
Raha zikiendelea.
Mdada huyu akionesha jinsi alivyofundishwa kukata nyonga.
BENDI inayoongozwa na vijana wadogo, Yamoto Band ambayo hivi karibuni imekuwa gumzo katika viwanja vya burudani kutokana na makamuzi yake, usiku wa kuamkia leo imefanya makamuzi ya nguvu na kuwadatisha vibaya mashabiki waliofurika kwenye Ufukwe wa Escape One jijini Dar es Salaam.
Katika burudani hiyo mashabiki walishindwa kuvumilia na kujikuta wakiacha viti na kuanza kujimwaya kila mmoja kwa jinsi alivyojisikia.