BENDI inayoongozwa na vijana wadogo, Yamoto Band ambayo hivi karibuni imekuwa gumzo katika viwanja vya burudani kutokana na makamuzi yake, usiku wa kuamkia leo imefanya makamuzi ya nguvu na kuwadatisha vibaya mashabiki waliofurika kwenye Ufukwe wa Escape One jijini Dar es Salaam.
Katika burudani hiyo mashabiki walishindwa kuvumilia na kujikuta wakiacha viti na kuanza kujimwaya kila mmoja kwa jinsi alivyojisikia.