Askofu Msaidizi wa Kanisa la la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Chediel Lwiza (kushoto) akitoa ibada fupi ya kumwombea marehemu.
Katikati ni mume wa marehemu, Ally Mwaiposa, mtoto wao Salimila Mwaiposa (kushoto) na Mektrida Mwaiposa (kulia).
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick (kushoto), Makamu wa Rais Dk. Mohammed Gharib Bilal (katikati) na Anne Makinda wakiwa katika maombolezo.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda, akisalimia waombolezaji wakati alipofika nyumbani wa marehemu Eugene jana.
MAKAMU wa Rais, Dk. Gharib Bilal, jana aliongoza mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Eugene Mwaiposa, huko Ukonga Kipunguni ‘A’ Matembele jijini Dar es Salaam ambako simanzi na vilio vilitawala miongoni mwa umati uliohudhuria huko akiwemo Waziri wa Serikali za Mitaa, Hawa Ghasia; Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Makongoro Mahanga na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda,.