Sunday, June 7, 2015

TASWIRA ZA MAZISHI YA MBUNGE EUGENE MWAPOSA UKONGA JIJINI DAR

Askofu Msaidizi wa Kanisa la la Kiinjili la Kilutheri Tanzania  (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Chediel Lwiza (kushoto) akitoa ibada fupi ya kumwombea marehemu.
Katikati ni mume wa marehemu, Ally Mwaiposa,  mtoto wao Salimila Mwaiposa (kushoto) na  Mektrida Mwaiposa (kulia).
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick (kushoto), Makamu wa Rais Dk. Mohammed Gharib Bilal (katikati) na Anne Makinda wakiwa katika maombolezo.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda, akisalimia waombolezaji wakati alipofika nyumbani wa marehemu Eugene jana.
...Akimfariji mume wa marehemu, Ally Mwaiposa.
Spika wa bunge la Tanzania Anna Makinda akisaini katika kitabu cha maombolezo jana.
Sehemu ya waombolezaji waliofika nyumbani kwa marehemu Eugene Mwaiposa huko  Ukonga Dar.
Baadhi ya watu waliosoma na marehemu nje ya Tanzania wakisoma risala ya maombolezo.
Baadhi ya waombolezaji waliofika mazishini.
Viongozi mbalimbali wa serikali wakiwa msibani.
MAKAMU wa Rais, Dk. Gharib Bilal, jana aliongoza mazishi ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ukonga, Eugene Mwaiposa, huko Ukonga Kipunguni ‘A’ Matembele jijini Dar es Salaam ambako simanzi  na vilio vilitawala miongoni mwa umati uliohudhuria huko akiwemo Waziri wa Serikali za Mitaa, Hawa Ghasia;  Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Makongoro Mahanga na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda,.