Jack
alisema, kwa muda aliodumu kwenye ndoa ameshaona raha na karaha yake
hivyo suala la kuolewa tena sasa hivi halipo akilini mwake.
“Katika
ndoa lazima kuwe na mabaya na mazuri, hata hivyo siwezi kusema ndoa ni
chungu hapana, ila mimi kwa sasa hivi nimeona nipumzike kwanza sitaki
tena ndoa labda kwa hapo baadaye nitakapojipanga tena upya,” alisema
Jack.
Jack alidumu na mumewe huyo kwa miaka miwili na nusu kabla
ya kupewa talaka hivi karibuni huku chanzo kikiwa ni kusalitiana katika
mapenzi.