Monday, February 2, 2015

LUNGI AFUNGUKIA NDOA YA SIRI

STAA wa sinema za Kibongo, Lungi Maulanga, amesema baada ya kufunga ndoa ya siri Novemba, mwaka jana na Jonson, Raia wa Cameroon, walidumu kwa muda mfupi kwenye ndoa na sasa wameachana.
Akifafanua undani wa sakata hilo, Lungi alisema alikubali kuolewa na mwanaume kwa ajili ya yeye kujipatia fedha na hakuwa akimpenda kwa dhati.
Staa wa sinema za Kibongo, Lungi Maulanga.
“Mimi mtoto wa mjini nilikuwa naye kwa sababu ana hela na nilijitoa fahamu hadi kufunga naye ndoa, lakini haikuwa kama halali kwa sababu yeye si Mtanzania na nilikuwa simpendi zaidi ya pesa zake tu, nimeshazipata, nimeachana naye,” alisema Lungi.